Psalms 114:1-6

Maajabu Ya Mungu Wakati Israeli Walipotoka Misri


1 aWakati Israeli walipotoka Misri,
nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,

2 bYuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu,
Israeli akawa milki yake.


3 cBahari ilitazama ikakimbia,
Yordani ulirudi nyuma,

4 dmilima ilirukaruka kama kondoo dume,
vilima kama wana-kondoo.


5 eEe bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia,
nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,

6 enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume,
enyi vilima, kama wana-kondoo?

Copyright information for SwhKC